Uchaguzi 2019: Waaustralia wanapiga kura katika uchaguzi wa shirikisho wenye mchuano mkali

Siku ya kupigia kura imefika wakati Waustralia wakipiga kwenye kura ili kuamua uamuzi wa bunge la shirikisho la nchi hiyo.

Voting

Voting Source: SBS

Vituo vya kupigia kura Australia vimefunguliwa kwa mamilioni ya wapiga kura kuchagua washindi na walioshindwa katika uchaguzi wa shirikisho 2019.

Zaidi ya milioni 16 wanatarajiwa kushiriki katika kura za kitaifa katika maeneo 7,000 ya kupigia kura nchini kote.

'Utakuwa usiku mrefu'

Scott Morrison Election 2019
Prime Minister Scott Morrison takes part in an election day sausage sizzle in Launceston, Tasmania. (AAP) Source: AAP
Kuanza siku ya uchaguzi, Waziri Mkuu Scott Morrison alizindua mradi wa mwisho kaskazini mwa Tasmania.

Bwana Morrison anatembelea vituo viwili vya kupigia kura kaskazini mwa Tasmania. Kisha atasafiri nyumbani kwa wapiga kura wa Sutherland Shire mjini Sydney, kabla ya kupiga kampeini na wabunge wengine wa Liberal katika viti vidogo mjini.


"Nadhani itakuwa usiku mrefu. Nimekuwa nikisema kuwa uchaguzi huu utakuwa wa mchuano mkali," Bwana Morrison aliiambia shirika la habari la Seven katika kipindi cha Sunrise leo Jumamosi.

"Wiki tano zilizopita watu hawakusema hivyo lakini siku zote nimetambua kuwa ni mchuano mkali," alisema.
 Labor Leader Bill Shorten starts election day.
Labor Leader Bill Shorten starts election day. Source: Getty
Kiongozi wa Labor Bill Shorten anatarajia kutembelea viti vinavyogombaniwa katika eneo la muhimu la ushindani la Victoria.

Bwana Shorten alianza siku kwa kukimbia mchakamchaka kuzunguka Melbourne huku akiwa amevaa fulana iliyokuwa na maandishi ya kauli mbiu "Piga kura 1 Mume wa Chloe Shorten".

"Ninachokijua baada ya siku 2000 katika kazi hii ni kwamba, nina ujasiri Labor itaweza kuendesha serikali ya umoja," aliiambia Sunrise.

Kiongozi wa upinzani alipiga kura katika wapiga kura wake wa Maribyrnong magharibi mwa Melbourne.

Kupiga kura-Mapema

ELECTION 2019
Bill Shorten vs Scott Morrison Source: Getty
Takriban kura za milioni 4.76 zimepigwa katika vituo vya kupiga kura vya mapema, na kura 700,000 zilipigwa Ijumaa, siku ya mwisho ya kampeni.

Hii inalinganisha na jumla ya kura milioni 2.5 katika hatua sawa ya uchaguzi wa shirikisho wa 2016.

Kwa kuongeza, kumekuwa na maombi ya kura milioni 1.5 za posta, Tume ya uchaguzi AEC walisema.

 


Share

Published

By Nick Baker
Presented by Frank Mtao

Share this with family and friends


Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service