Wataalam wana kadiria kuwa itagharimu maeneo husika ya mafuriko hayo ma bilioni yama dola, kukarabati miundombinu mhimu iliyo haribika, bila kutaja mali za watu zilizo potea nakuharibika katika tukio hilo.
Jimboni Queensland Mama Idrissa alieleza Idhaa ya Kiswahili ya SBS kwamba, "nguo zote za watoto zime haribika, carpet ndani ya nyumba ime lowa, na itabidi nitupe vitu vingi ambavyo vimeharibiwa na maji pamoja nakusafisha kila sehemu ili kuondoa uchafu na harufu mbaya ambayo ime jaa ndani ya nyumba. Pia itabidi nitupe kila kitu ambacho kiko ndani ya friji kwa sababu vyote viliharibika baada ya umeme kukatwa kwa zaidi ya siku tatu".

Maafisa wa jeshi la Ulinzi wa Australia, wasaidia katika shughuli yausafi baada ya mafuriko kusababisha uharibifu mkubwa mjini Lismore. Source: AAP / Jason O'Brien