Licha ya umaarufu wa mchezo wa Tennis duniani, ni nadra kuona mchezaji mwenye asili ya Afrika Mashariki, akishiriki katika michuano mikubwa ya mchezo wa tennis duniani.
Angella Okutoyi binti mwenye asili ya Kenya, alibadili hali hiyo katika viwanja vya tennis mjini Melbourne, Victoria ambako, alipeperusha bendera ya Kenya na Afrika Mashariki kwa fahari kubwa, nakuwaacha wapinzani wake pabaya.

Alipozungumza na Idhaa ya Kiswahili ya SBS, Angella alitueleza jinsi mjomba wake alivyo mshawishi nakumfunza kucheza tennis akiwa na umri wa miaka minne, mipango yake yakuwa mchezaji wakulipwa wa tennis, pamoja na maono yake kwa siku za usoni katika tennis.
Angella alishinda mechi mbili nakupoteza mechi moja katika michuano ya wachezaji chipukizi. Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.
Share






