Kombe la mataifa ya jamii zawana Afrika wanao ishi jijini Sydney, linatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa mwaka huu kuliko miaka ya nyuma.
Moja ya mataifa yanayo shiriki katika kombe hilo ni Sudan Kusini, ambayo inavijana wengi wenye vipaji na moyo wakujituma katika mechi.
Nahodha wa Sudan Kusini Athiei, alieleza Idhaa ya Kiswahili ya SBS wakati wa sherehe ya uzinduzi wa michuano hiyo kuhusu maandilizi ya timu yake, na alizungumzia pia hoja kuhusu 'hofu' ambayo timu nyingi hukabili wanapo ratibiwa kucheza dhidi yao.
Michuano hiyo itaanza tarehe 7 Novemba 2020, katika uwanja wa Progress, South Granville, New South wales.
Share






