Australia yajiunga katika mkataba mkubwa wa biashara duniani

Waziri Mkuu Scott Morrison akiwa pamoja na Waziri wa Biashara Simon Birmingham

Waziri Mkuu Scott Morrison akiwa pamoja na Waziri wa Biashara Simon Birmingham, baada yakutia saini mkataba wa biashara wa RCEP, jijini Canberra, Australia Source: AAP Image/Lukas Coch

Australia imetia saini mkataba mkubwa sana wa biashara, ambao umechukua miaka minane kuafiki, nakushirikisha nchi 14 kutoka kanda ya Asia-Pacific.


Biashara za Australia, vyuo pamoja na wanao toa huduma ya afya, wanatarajiwa kufaidi kupitia mkataba huo, wakati huo huo serikali ya shirikisho inajaribu kuboresha mahusiano yake na China.

Kando na biashara ya bidhaa, maafikiano hayo yanatoa sheria sawia kwa biashara yakidijitali, pamoja na haki miliki.Mkataba huo pia utatoa upatikanaji bora kwa sekta za huduma za Australia kama, huduma zakifedha, huduma ya afya pamoja na elimu.

Makundi yakibiashara nayo yamesema kuwa mkataba huo wakibiashara ni muhimu, kwa uponaji wa Australia kutoka kutikisishwa kwa uchumi ambako kulisababishwa na janga la COVID-19.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service