Mafuriko ya tsunami na tetemeko la ardhi ya Indonesia, yameathiri pia hapa Australia kwa wale wenye ndugu na marafiki wanaoishi kwenye maeneo ya maafa. Jumuiya na watoa misaada nchini Australia, wameunda vikosi kazi kuhakikisha kunapatikana misaada ya dharura kwa haraka iwezekanavyo, iende kwenye maeneo yalioathirika. Taarifa ifuatayo inayoletwa kwako na Frank Mtao, inafafanua zaidi...
Share






