Wa Australia wa kwama katika machafuko Uganda

Mikono juu: vyombo vya usalama vyaendeleza kamata kamata mjini Kampala, Uganda

Wakazi waondolewa jengoni waki inua mikono, vyombo vya usalama viki endeleza msako wa waandamanaji mjini Kampala, Uganda Source: AAP

Uganda imetumbukia katika machafuko ya uasi wa raia, na vyombo vya usalama vime pewa mtihani toka kwa raia ambao wana andamana, wakitaka msanii maarufu ambaye pia ni mwanasiasa Robert Kyagulanyi maarufu kwa jina la Bobi Wine, na wabunge wenzake pamoja na wanaharakati ambao wame wekwa vizuizini waachiliwe.


Jumatatu polisi wa Uganda walifyatua risasi nakutumia gesi zakutoa machozi, kuwatawanya waandamanaji ambao wanataka msanii maarufu ambaye ni mwanasiasa pia Bobi Wine, ambaye amekuwa mkosoaji mkuu wa Rais Yoweri Museveni aachiwe huru, pamoja na wabunge wenzake na wanaharakati walio kamatwa pia.

Polisi wa Uganda wame thibitisha kuwa wamekamata watu wapatao 103, ambao walihusika katika maandamano baada ya mbunge Robert Kyagulanyi na wabunge wenzake pamoja na wanaharakati kuwekwa vizuizini. Imeripotiwa pia, kuwa mtu mmoja ame uawa katika maandamano hayo.

SBS Swahili ilizungumza na mgombea wa zamani wa udiwani katika halmashauri ya jiji la Logan, Queensland, Blaise Itabelo kuhusu hali ilivyo mjini Kampala, Uganda.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service