Imethibitishwa kuwa mshauri mkuu wa Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza ambaye pia ndiye kiongozi wa vyombo vya habari, mawasiliano ya taarifa Willy Nyamitwe, amepona jaribio dhidi ya maisha yake, ila baadhi ya walinzi wake walijeruhiwa namwingine amefariki katika shambulizi hilo.
Bw Nyamitwe amethibitisha kupitia Twitter kuwa yuko salama na anaendelea kupokea matibabu katika hospitali moja ambayo haija tambuliwa.
SBS Swahili ilizungumza na mwandishi wetu Ramadhani Kibuga ambaye alitupasha taarifa zaidi kuhusu tukio hili kutoka Bujumbura, Burundi.
Share
