Canberra: tathmini ya wiki hii 17 Agosti 2018

Seneta Fraser Anning na kiongozi wa waislamu wa Australia Dkt. Ibrahim Abu Mohamad

Seneta Fraser Anning akitoa hotuba yake ya kwanza, na kiongozi wa waislamu wa Australia Dkt. Ibrahim Abu Mohamad achangia katika ukosoaji wa hotuba hiyo. Source: AAP

Baada ya wiki sita ya mapumziko ya majira ya baridi, wanasiasa wa shirikisho wame rejea mjini Canberra ambako utata ulitawala siasa ya taifa.


Seneta mmoja ambaye alikuwa hajulikani sana, kabla atoe hotuba yake ya kwanza ndani ya seneti, alijipa umaarufu nchini kote kwaku pendekeza marufuku ya wahamiaji ambao ni waislamu.

Wakati huo huo sera muhimu ya serikali kwa nishati, ilipita kizuizi cha kwanza kwaku kubaliwa katika mkutano wa chama tawala.

Hotuba ya seneta huyo pamoja na sera ya nishati ya serikali, zili zua utata hata kama swala moja lilifunika lingine kwa ukali wa ukosoaji.

Wakati wanachama wa serikali ya mseto, wanaweza piga kura kwa hiari yao, itaonekana vibaya kwa serikali iwapo baadhi yao wata vuka sakafu kupiga kura dhidi ya sera ya dhamana ya nishati.

Muswada huo unatarajiwa kufikishwa bungeni, katika vikao vya kwanza viwili, utakapo idhinishwa na serikali za mikoa na majimbo.

 


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service