Canberra: tathmini ya wiki hii 20 Septemba 2019

Waziri Mkuu wa Australia Scott Morrison apewa zawadi toka kwa Waziri Mkuu wa Fiji Frank Bainimarama

Waziri Mkuu wa Australia Scott Morrison apewa zawadi toka kwa Waziri Mkuu wa Fiji Frank Bainimarama Source: AAP

Ziara ya waziri mkuu wa Fiji, tathmini kwa mfumo wa sheria ya familia na shinikizo ya ziada kwa mbunge wa chama cha Liberal Gladys Liu ambaye amezingirwa kwa utata, vilikuwa baadhi ya maswala yaliyo tawala wiki hii katika siasa za shirikisho.


Serikali ya Morrison pia ilipigia debe ziada ya bajeti ambayo chama cha Labor imesema, inakuja kwa gharama ya uwekezaji kwa mfumo wa dhamana ya ulemavu wakitaifa.

Wiki hii pia waziri wa maswala ya nyumbani Peter Dutton aliwasilisha sheria bungeni, yenye lengo lakufanya iwerahisi kufuta uraia wa mtu ambaye ana uraia wa nchi mbili, ambaye amepatwa na hatia ya makosa ya ugaidi.

Ila mtumishi wa umma mwenye wajibu wakufuatilia sheria za ulinzi wa Australia James Renwick alisema kwamba, sheria hiyo haija dhibitiwa kwa hali yake ya sasa na ameomba ifutwe.

Wakati huo huo waziri mkuu Scott Morrison amemaliza wiki hii akiwa nchini Marekani, ambako anakutana na rais wa Marekani Donald Trump, pamoja na maafisa wengine wa ngazi za juu katika ikulu ya Marekani.

Bunge litakuwa katika mapumziko kati ya Septemba 20 hadi Oktoba 7 2019.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service