Katika siku za hivi karibuni, wanasiasa na baadhi ya vyombo vya habari nchini Australia, wame kuwa wakiongoza mjadala kuhusu vikundi vya vijana wakiafrika wanao fanya vurugu mjini Melbourne, naku inyima jamii pana fursa yaku shiriki katika shughuli zao za kila siku kwa sababu yaku jawa uoga.
Madai hayo yame sababisha kundi la vijana mjini Melbourne kuandaa tamasha ya "Ujamaa Community Festival", ambako wanachama wa jamii zawa Afrika walikutana na wenzao kutoka jamii pana yawa Australia, kuzungumza, kuchangia uzoefu wao pamoja nakusherehekea utofauti wa jamii zinazo ishi Victoria.
SBS Swahili ilizungumza na mmoja wa vijana aliye hudhuria tukio hilo. Katika mahojiano alizungumzia umuhimu wa tukio hilo, na alichangia pia baadhi ya pendekezo ambazo anahisi zinaweza badili gumzo inayo ongozwa na wanasiasa na vyombo vya habari ambavyo vime kuwa viki shinikiza vijana waki Afrika wa Melbourne.
Share






