D R Congo yawalisha fimbo vijana wa Farao

Vijana wa DR Congo washerehekea goli

Vijana wa DR Congo, washerehekea goli dhidi ya Misri katika kombe la Afrika jijini Sydney, Australia Source: SBS Swahili

Mechi za kwanza za kombe la Afrika zime anza naku kamilika kwa kishindo katika viwanja vya mazoezi vya Western Sydney Wanderers mjini Rooty Hill, New South Wales, Australia.


Vijana wa D R Congo wali ingia dimbani dhidi ya Misri katika mechi ambayo, kihistoria huwa na changamoto zake na licha ya DR Congo kumaliza kipindi cha kwanza wakiwa na ushindi wa goli moja kwa sufuri, vijana wa Misri walionesha umahiri wao kwa kuzuia miamba ya DR Congo kuwatatiza.

Kipindi cha pili cha mechi hiyo kilianza sawia na kile cha kwanza, hali ambayo ilianza kuzua tumbo joto miongoni mwa mashabiki wa timu hizo mbili. Licha ya pandashuka za mechi hiyo, vijana wa DR Congo walionesha umahiri wao nakushinda mechi hiyo kwa magoli 4 kwa 1 ya Misri.

Punde baada ya mechi hiyo kuisha, mashabiki pamoja na nahodha wa DR Congo wali eleza Idhaa ya Kiswahili ya SBS hisia zao kwa mechi hiyo. Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service