Zoezi la kutafuta miili ya watu waliopoteza maisha linaendelea katika mji wa Uvira, mkoani Kivu Kusini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya kukumbwa na mafuriko katikati mwa wiki iliyopita.
Imeripotiwa kuwa takriban zaidi ya watu 65 walipoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa, huku nyumba kadhaa zikisombwa na maji.
Delphin, ndiye rais wajamii yawatu kutoka Congo wanao ishi nchini Australia, ame eleza Idhaa ya Kiswahili ya SBS kile ambacho viongozi wa jamii wanafanya kuwasaidia wanachama wao nchini Australia pamoja na jamaa wao ambao wame athirika nchini Congo.
Share





