Malumbano ya uongozi ndani ya chama tawala, yame tikisa imani ya umma ya Australia. Wengi wao wakisema wame choshwa na mivuto, ya mawaziri ambao wanaweka maslahi yao, mbele ya maslahi ya taifa.
Wakati kundi moja la wabunge namaseneta wa chama cha Liberal, walikuwa wakiongoza kampeni yakubadili kiongozi wa chama, ambaye pia ndiye waziri mkuu wa taifa, wabunge wengine namaseneta, walijipata wamezolewa na wimbi la vurugu iliyo ibuka.
Lucy Gichuhi ni Seneta wa jimbo la Kusini Australia wa chama cha Liberal, alishuhudia kwa hali yakipekee jinsi mirengo yakulia nakushoto, ya chama tawala ilivyokuwa ikijiangamiza.
Kwa makala mengine kama haya, tembelea tovuti yetu: sbs.com.au/swahili
Share






