George afunguka kwa nini alikimbia kutoka Adelaide hadi Melbourne

George (akivaa kofia) na washirika wa kampeni yake.jpg

George Chijarira ni mwanachama wa jumuiya ya watanzania wanao ishi Melbourne, Victoria.


Siku chache zilizo pita, alishiriki katika kampeni yaku elimisha umma kuhusu ugonjwa wa Usonji (Autism).

Kwa mujibu wa shirika la Afya duniani (WHO):
Ugonjwa wa Usonji kwa kiingereza Autism, ni ugonjwa ambao hukumba mtoto mmoja kati ya kila watoto 160 duniani. Usonji ni tatizo la kibaiolojia analopata mtoto anapokuwa tumboni mwa mama yake, na dalili huonekana kuanzia umri wa miaka mitatu na kuendelea. Kabla ya hapo wataalamu wanasema ni aghalabu kuona dalili hizo ambapo zinapojitokeza mtoto hukosa mbinu za uhusiano, anashindwa kuzungumza na wakati mwingine kurukaruka na hata kujing’ata."
Bw George ni mzazi wa mtoto mwenye Usonji, na hiyo ilikuwa moja ya sababu kubwa iliyo mshawishi kushiriki katika kampeni hiyo, kando na uchochezi kutoka kwa baadhi ya marafiki wake.


George akiwa na mwanae, aliye mpa motisha ya kukimbia kutoka Adelaide hadi Melbourne.
Bonyeza hapo juu kwa mahojiano kamili, nakusikia jinsi George alivyo jiandaa kuelimisha umma kuhusu ugonjwa wa Usonji kwa kukimbia kutoka Adelaide hadi Melbourne.
George apepea bendera ya kampeni yake.jpg
Kwa taarifa zaidi kuhusu kampeni ya Bw George tembelea: www.georges-run.com

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
George afunguka kwa nini alikimbia kutoka Adelaide hadi Melbourne | SBS Swahili