Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Germain:"Kunawatu wanataka angamiza Kamerhe kisiasa"

Vital Kamerhe azungumza na waandishi wa habari

Vital Kamerhe azungumza na waandishi wa habari Source: Junior D. Kannah

Mkuu wa ofisi ya rais wa DRC, Vital Kamerhe amezuiwa ndani ya jela kuu la Makala mjini Kinshasa.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS


Share this with family and friends


Mkuu wa ofisi ya rais wa DRC, Vital Kamerhe amezuiwa ndani ya jela kuu la Makala mjini Kinshasa.


Bw Kamerhe amezuiwa kwa tuhuma za ufisadi wa fedha zilizo tengwa kwa ajili yakutekeleza mpango wa siku 100 za rais Félix Tshisekedi.

Vital Kamerhe anashukiwa kwa kosa la ubadhirifu wa fedha za serikali, ila wafuasi wa UNC wanamatumaini na sheria ya Kongo, licha ya kuwa wamekerwa kuona kiongozi kama huyo ametupwa jela badala ya kuwekwa chini ya ulinzi katika kizuizi cha nyumbani.

Licha yakusalia gerezani kwa siku kadhaa, Bw Kamerhe amekana shutma zote dhidi yake. Germain Byadu ndiye kiongozi wa chama cha UNC nchini Australia. Katika mahojiano na Idhaa ya Kiswahili ya SBS, Bw Byadu aliweka wazi masaibu yanayo mkumba kiongozi wa chama chake.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now