Serikali ya Berejiklian imesalia mamlakani jimboni New South Wales, hatua ambayo imempa Gladys Berejiklian sifa yakuwa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kuongoza jimbo hilo.
Wakati hesabu za kura zinaendelea jimboni kote, inaonekana kama serikali ya mseto imeshinda viti 46 kati ya viti 47 ilihitaji, kumaanisha itarejea mamlakani kama serikali ya wachache.
Iwapo hawata pata kura zakutosha, Bi Berejiklian tayari amepata ahadi za kusaidiwa na wabunge huru watatu wanao rejea bungeni.
Ushindi huo unaonekana kama ushindi wa wanawake pamoja nakuipiga jeki serikali ya mseto ya shirikisho, miezi miwili kabla ya uchaguzi washirikisho.
Share






