Hoja za afya, na usalama wa mipaka zafungua wiki ya pili ya kampeni ya uchaguzi mkuu

Waziri Mkuu Scott Morrison na Kiongozi wa Upinzani Anthony Albanese.

Waziri Mkuu Scott Morrison na Kiongozi wa Upinzani Anthony Albanese. Source: SBS

Wiki ya pili ya kampeni za uchaguzi mkuu zime tumbukia katika vita vya kampeni zakutisha kati ya vyama viwili vikubwa nchini.


Scott Morrison na Anthony Albanese walipo tembelea maeneo bunge mhimu, mada za ulinzi wa mipaka na maswala ya huduma ya afya yalikuwa juu ya ajenda zao.

Waziri Mkuu na Kiongozi wa Upinzani walitembelea maeneo bunge mhimu jana Jumatatu. Scott Morrison akiwa Magharibi Australia ambako chama cha Liberal, kilishindwa vibaya katika uchaguzi wa jimbo hilo mwaka jana. Alitembelea pia eneo bunge la Pearce, ambalo lilikuwa chini ya uongozi wa mbunge anaye staafu Christian Porter. Hiyo ilikuwa ziara ya tatu ya waziri mkuu jimboni humo katika muda wa zaidi ya mwezi mmoja.

Wakati huo huo Anthony Albanese anajua anakazi ya ziada jimboni Queensland, ambako chama cha Labor kiliteseka sana katika uchaguzi mkuu uliopita. Katika wiki zijazo wawili hao wataendelea kutembelea maeneo bunge ambayo lazima vyama vyao vishinde katika uchaguzi mkuu.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Hoja za afya, na usalama wa mipaka zafungua wiki ya pili ya kampeni ya uchaguzi mkuu | SBS Swahili