Matatizo ya misaada ya kibinadamu kwa ajili ya tetemeko la ardhi kisiwani Sulawesi yanaendelea kuwa mabaya zaidi. Zaidi ya watu 1,400 wameripotiwa kuwa wamekufa kutokana na tetemeko kubwa la ukubwa wa 7.5 na tsunami iliyofuata, ilikipiga kisiwa hicho cha Indonesian siku ya Ijumaa. Takribani watu 2,500 wamejeruhiwa na 113 hawajulikani walipo. Mwandishi wetu Frank Mtao ametuandalia taarifa ifuatayo...
Share






