Wakati wakulima wanaendelea kukabiliana na madhara ya ukame katika ukanda wa Australia, taasisi za elimu katika maeneo husika, nazo zimelazimishwa kutafuta mikakati mbadala, yakuwasaidia nakuhakikisha wanafunzi wao wanaendelea na elimu yao katika taasisi zao.
Dr Ndungi Wa Mungai na Dr Kiprono Langat kutoka chuo cha Charles Sturt mjini Wagga Wagga, walieleza Idhaa ya Kiswahili ya SBS jinsi wanawasaidia wanafunzi kutoka maeneo ambayo yame athiriwa kwa ukame.
Share





