Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Ibada za alfajiri zakumbuka mchango wa waAustralia katika migogoro

Jua lachomoza katika eneo la Point Perpendicular wakati wa ibada ya siku ya Anzac kwenye eneo la HMAS Creswell, Jervis Bay in NSW.

Jua lachomoza katika eneo la Point Perpendicular wakati wa ibada ya siku ya Anzac kwenye eneo la HMAS Creswell, Jervis Bay in NSW. Source: Australia Department of Defence

Maelfu yawa Australia walijumuika kutoa heshima zao kwa wanajeshi katika ibada za alfajiri za siku ya Anzac, ambako viongozi wa nchi walitambua pia vita vya uhuru vya Ukraine.


Jua linapo chomoza katika siku ya ANZAC, mlio unao fahamika wa tarumbeta huwaleta wa Australia na watu wa New Zealand pamoja kote nchini na duniani kuwakumbuka walio potezwa katika vita.

Ilikuwa miaka 107 iliyopita leo (Jumatatu 25 Aprili 2022) wanajeshi wa Australia na New Zealand walipo tua katika eneo la Gallipoli nchini Uturuki katika vita vya kwanza vya dunia. Wanajeshi hao wanao julikana kwa jina la ANZACs, walishindwa miezi minane baadae baada, yakukabiliwa kwa magumu mengi pamoja na majeruhi wengi.

Ibada hizo zilifuatwa na gwaride zamaveterani pamoja na shughuli zingine zaukumbusho kama ilivyo tamaduni. Ng’ambo, sherehe za ukumbosho zitafanywa nchini Ufuransa, Uturuki, Thailand, Malaysia, na Papua New Guinea.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now