WaTanzania walio nje na nchini wame shangazwa na uamuzi unao toka katika serikali iliyo ingia madarakani kwa shangwe na matumaini mengi.
Waziri mmoja maarufu alifutwa kazi na wadhifa wake kupewa mwingine chini ya masaa 24 baadae, wakati huo huo msanii maarufu alikamatwa nakuachiwa huru bila kufunguliwa mashtaka baada yaku toa wimbo ulio kosoa uongozi na hali ya maisha nchini Tanzania.
SBS Swahili ilizungumza na baadhi ya watanzania wanao ishi Australia, kuhusu mvutano unao endelea nchini mwao.
Share





