Ujumbe wa shukrani na pongezi umetolewa kwa kiongozi wa NSW Mike Baird ambaye ametangaza ghafla kuwa anastaafu kutoka siasa, katikati ya muhula wake wa pili kama kiongozi.
Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 48, alisema kwamba maswala ya afya ya familia yake yalichangia pakubwa katika uamuzi wake.
Wiki ijayo Chama cha Liberal kitamchagua kiongozi mpya, na imedokezwa kuwa mweka hazina wa NSW Gladys Berejiklian atamrithi Bw Baird wadhifa wake.
Share
