Jamii zawa Australia wenye asili ya Afrika, wanastahili adhimisha siku kuu ya Australia aje?

Dr Casta Tungaraza azungumza na SBS Swahili

Dr Casta Tungaraza azungumza na SBS Swahilim, kuhusu maadhimisho ya siku kuu ya Australia Source: SBS Swahili

Tarehe 26 January huadhimishwa kama siku kuu ya Australia, ni wakati ambapo ina aminika kuwa meli za kwanza zawangereza ziliwasili katika bandari ya Jackson, jimboni NSW katika mwaka wa 1788 nakuinua bendera ya Uingereza.


Siku hiyo huadhimishwa nchini Australia kwa sherehe tofauti pamoja na maandamano, yanayo ongozwa na wanaharakati wa jamii zawa Aboriginal na wanavisiwa wa Torres Strait, ambao ndiwo wa Australia wakwanza ambao wanataka tarehe hiyo ibadilishwe kwa sababu ya maovu ambayo wakoloni walifanyia jamii zao.

Dr Casta Tungaraza ni mwenyekiti wa bodi inayo toa ushauri wa maswala ya biashara na uhusiano, kati ya Australia na Bara la Afrika katika idara ya maswala ya kigeni ya serikali ya madola ya Australia. Dr Tungaraza pia ndiye mwanzilishi wa shirika la umoja wa wanawake nchini Australia.

Alishiriki katika ibada maalum ya tarehe 26 Januari, ambayo iliandaliwa na jamii yawa Aboriginal na wanavisiwa wa Torres Strait. Ibada hiyo ilipeperushwa katika runinga nchini Australia nakimataifa. Dr Tungaraza ali eleza SBS Swahili jinsi anahisi jamii yawa Afrika wanao ishi nchini Australia, wanastahili adhimisha siku kuu ya Australia (26 Januari).

 


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service