Kenya kushuriki katika kombe la Afrika mjini Sydney kwa mara ya kwanza

Abed, nahodha wa Kenya mjini Sydney, Australia

Abed, nahodha wa Kenya mjini Sydney, Australia Source: SBS Swahili

Jamii zenye asili ya Afrika zimekuwa ziki shiriki katika michuano ya soka, ya kombe la Afrika kwa miaka mingi mjini Sydney, Australia.


Hata hivyo, Kenya haija wahi wakilishwa katika michuano hiyo, licha ya jamii hiyo kuwa na vijana wengi wenye uwezo mkubwa waku cheza soka.

Hatimae baada ya miaka mingi yaku hojiwa kwa nini Kenya haiwakilishwi katika michuano hiyo, vijana wa Kenya wametoa jibu hilo kwa kusajili timu yao, na masaa machache yajao Kenya itaingia dimbani dhidi ya Burkina Faso katika michuano ya Kombe la Afrika mjini Sydney, Australia.

Katika mazungumzo maalum katika hafla ya uzinduzi wa michuano hiyo, nahodha wa timu ya Kenya Bw Abed, alieleza Idhaa ya Kiswahili ya SBS jinsi kikosi chake kimejiandaa pamoja na matarajio wanayo wanapo anza safari yao katika michuano hiyo.

 

Mechi ya Kenya ita anza saa saba mchana tarehe 7 Novemba 2020, katika uwanja wa Progress, South Granville, New South Wales, Australia.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service