Kwibuka25:"Lazima tujifunze kukubali tofauti zetu, nakuishi pamoja kwa amani"

Rais Kagame na viongozi wenza washiriki katika sherehe yaku kumbuka mauaji ya kimbari nchini Rwanda

Rais Kagame na viongozi wenza washiriki katika sherehe yaku kumbuka mauaji ya kimbari nchini Rwanda Source: EPA

Rwanda na raia wake duniani kote wanaadhimisha kumbukumbu ya miaka 25 ya mauaji ya Kimbari, ambapo watu wapatao 800,000 hasa wa kabila la Watutsi waliuawa.


Miezi mitatu ya mauaji ilishuhudiwa nchini humo miaka 25 iliyopita, katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Rwanda, ambavyo vilidai maisha mengi pamoja nakufanya watu wengi kutawanyika nje ya nchi hiyo nakuwa wakimbizi.

Maadhimisho ya Jumapili ni mwanzo wa wiki nzima yamatukio, yenye lengo lakuwakumbuka walio uawa. Inakadiriwa kuwa idadi yawatu elfu 10 wali uawa kila siku na asilimia 70 ya watu kutoka kabila la wachache la watutsi wali uawa pamoja, na zaidi ya asilimia 10 ya watu nchini humo, kabla ya vita hivyo kumalizika mwezi Julai 1994.

SBS Swahili ilihudhuria ibada iliyo andaliwa na jamii yawanyarwanda wanao ishi NSW, Australia ambako walifanya maadhimisho ya miaka 25 ya mauaji hayo ya kimbari. Bofya hapo juu kusikiza mazungumzo tuliyo fanya na baadhi ya wahanga wa mauaji hayo pamoja na viongozi wa jamii hiyo.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service