Chama cha Labor kime ahidi familia zote nchini Australia kuwa, zita okoa mamia ya dola kila mwaka chini ya mpango wayo waku zuia ongezeko la gharama ya bima ya afya binafsi.
Kiongozi wa upinzani Bill Shorten amesema pendekezo laku zuia ongezeko la malipo hayo lina onesha chama cha Labor ndicho chama ambacho kina mpango waku kabiliana na shinikizo ya ongezeko ya gharama ya maisha.
Chama cha afya ya umma nchini Australia kimekaribisha pendekezo la uwepo wa tume ya uzalishaji, chama hicho kimesema malipo yame kuwa yaki ongezeka pamoja na sera kwa watu binafsi, makampuni ya bima binafsi yamekuwa yakipata faida kubwa wakati huo huo yana kandamiza mfumo wa Medicare.
Share






