Barabara nyingi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ziko kavu, na hakuna ishara nyingi za shughuli katika miji ya taifa hilo la ukanda wa Afrika ya Kati.
Vyama vya upinzani vinaongeza shinikizo dhidi ya Rais Kabila ajiuzulu, baada ya muda wake rasmi wa uongozi kukamilika.
Serikali ya Rais Kabila imejibu shinikizo hilo kwaku tangaza kuundwa kwa serikali mpya ambayo imejumuisha viongozi kadhaa wa upinzani.
Kwakupata uelewa zaidi wa hali inavyo endelea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, SBS Swahili ilizungumza na mwandishi wetu Byobe Malenga.
Share
