Wiki ili Bajeti ya mwaka wa fedha wa 2017-18 ilitawala mjadala nchini kote. Serikali ilikuwa ime toa fununu kuhusu yatakayo jumuishwa ndani ya bajeti hiyo na hatimae bajeti ilisomwa rasmi usiku wa Jumanne tarehe 9 mei 2017.Aliposoma bajeti hiyo, mweka hazina wa shirikisho Scott Morrison alisema bajeti hiyo ina husu uamuzi sahihi, pamoja naku boresha siku za usoni.
Masaa machache kabla yakusomwa kwa bajeti ya taifa, Bi Lucy Gichuhi ali apishwa ndani ya Seneti ya shirikisho, baada ya wiki kadhaa za vuta ni kuvute kati yawanasheria wake, na wanasheria wa serikali na chama cha upinzani ndani ya mahakama kuu.
Mvutano huo ulizuka baada ya aliyekuwa kiongozi wa chama cha Family First Bob Day kuvuliwa useneta wake na vyama vingine kuhoji uhakiki wa Bi Gichuhi kuhudumu kama seneta kwa sababu ya uraia wake.
Hata hivyo mahakama kuu iliamua Bi Gichuhi anastahili kuhudumu kama Seneta, na hatimae Jumanne aliapishwa kuwa Seneta mpya huru wa Kusini Australia baada yaku jiondoa ndani ya chama cha Family First siku chache kabla.
Share





