Kwa muda mrefu wakaaji wa kitongoji cha Goodna, Queensland wame kuwa waki imba sifa za mgahawa wa Bi Esther kwa jina la Mama Nitiliye.
Hatimae SBS Swahili ilifika katika mgahawa huo kuji thibitishia sifa na maoni ambayo ilikuwa iki pokea mara kwa mara kutoka kwa wateja na wapenzi wa vyakula vya mgahawa huo.

Bi Esther alitupokea nakutueleza kilicho mpa moyo waku anzisha mgahawa huo pamoja na mapokezi ya vyakula anavyo uza, na jinsi alivyo kabiliana na changamoto ya amri zakubaki ndani wakati wa kilele cha UVIKO-19 jimboni Queensland.
Bonyeza hapo juu kwa mahojiano kamili.
Share






