Msimu mpya wa ligi kuu ya England unaendelea kuwashangaza mashabiki wa timu zinazo shiriki.
Manchester United walikuwa wenyeji wa Tottenham Hotspur FC ambao mwalimu wao Jose Mourinho ni mwalimu wa zamani wa Manchester United.
Katika mechi ya msimu uliopita kati ya timu hizo mbili, wenyeji waliibuka washindi, ila mreno huyo alikuwa na mipango tofauti kwa mechi ya msimu huu.
Mwanaspoti wetu Frank Mtao, alizungumza na Gode Migerano kuhusu hali inavyo endelea, katika ligi kuu ya mpira wa miguu ya England.
Share






