Zaidi yawa Australia elfu moja, watambuliwa katika tuzo za siku kuu ya Australia

Washindi wa tuzo yawa Australia wa 2019 wapigwa picha wakiwa na waziri mkuu Scott Morrison

Washindi wa tuzo yawa Australia wa 2019 wapigwa picha wakiwa na waziri mkuu Scott Morrison Source: AAP

Zaidi ya idadi yawa Australia takriban elfu moja, wame tambuliwa kwa michango yao mizuri katika jamii zao.


Orodha ya walio tuzwa mwaka huu, ni kubwa zaidi katika historia ya tuzo za Australia, na watu takriban mia mbili watakao pokea tuzo hizo mwaka huu, walizaliwa ng'ambo.

Wanaume wawili walio shiriki katika oparesheni ya uokoaji wa wavulana 12 pamoja na mkufunzi wao wa soka, katika mapango yaliyo kuwa yame furika nchini Thailand mwaka jana, walitangazwa kuwa wa Australia wa mwaka wa 2019. Dr Craig Challen na Dr Richard Harris ambao ni marafiki wa muda mrefu, walikuwa wanajiandaa kuenda likizoni, walipo pokea ombi lakusaidia katika oparesheni ya uokoaji wa timu hiyo ya soka.

Wawili hao waliporejea nchini, walipewa tuzo la Nyota ya Ujasari, ambayo ni tuzo ya pili kwa umuhimu ya ujasiri nchini Australia.Kwa watu wengi, tuzo hiyo ni tazamio baada ya miaka mingi ya huduma, nakutoa michango katika njia zao tofauti.Ila wanacho changia ni nia yaku toa mchango, kadri ya uwezo wao kwa jamii zao.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service