Mgogoro wa moto wa vichaka unao endelea katika majimbo ya New South Wales na Queensland, umezua vita vya maneno kisiasa kuhusu kama kutokuchukua hatua kwa mabadiliko ya tabianchi kumesababisha janga hilo.
Naibu waziri mkuu amewakashifu wakosoaji wa sera zake, akisema ni wehu wanao ishi katika maeneo ya ndani ya jiji.
Ila madai hayo yame wakasirisha wanao athiriwa moja kwa moja na janga hilo la moto.
Hata hivyo, inaonekana kama siasa za mabadiliko ya tabianchi, zitaendelea kuchemka katika msimu wa majira ya joto, wakati tisho la moto wa vichaka likiendelea kuongezeka.
Share





