Wazazi wengi hujitahidi kuwatuma watoto wao ng'ambo, kufanya elimu ya juu kwa matumaini kuwa watoto hao watafanikiwa nakusaidia familia zao pia.
Hata hivyo, ni taarifa gani ambazo wazazi hao hupewa, kuhusu sehemu watoto wao wana enda, pamoja na changamoto ambazo watoto wao watakabiliana nazo wakiwa mbali ya familia zao?
SBS Swahili ilizungumza na Bi Nany Kamau Birgen, aliye chapisha video akizungumzia baadhi ya changamoto zinazo wakabili, wanafunzi wanao wasili nchini Australia kwa elimu. Video hiyo imesambaa mtandaoni nakuzua gumzo kali ndani ya jamii. Bofya hapo juu kwa mahojiano kamili.
Share






