Washindi wa tuzo ya amani ya Nobel, wasema 'tuzo wanayo taka tu ni haki'

Dkt Denis Mukwege kutoka DRCongo na Nadia Murad kutoka Iraq waonesha tuzo zao za amani za Nobel

Dkt Denis Mukwege kutoka DRCongo na Nadia Murad kutoka Iraq waonesha tuzo zao za amani za Nobel mjini Oslo, Norway. Source: NTB scanpix

Wapokeaji wa pamoja wa tuzo ya amani ya Nobel ya mwaka wa 2018, wame tumia hotuba zao zaku kubali tuzo hiyo, kumulika swala la unyanyasaji wa kingono ambao wanawake na watoto wengi hupitia, katika maeneo ya vita duniani kote.


Nadia Murad na Dkt Denis Mukwege walipokea tuzo hizo katika sherehe iliyo andaliwa nchini Sweden ila, wawili hao wamesema kazi yao ya uanaharakati bado ita endelea.

Uamuzi waku mulika kampeni dhidi ya unyanyasaji wakingono, ulijiri baada ya tuzo ya maandishi ya nobel kuahirishwa kwa sababu ya kashfa ya ubakaji. Jean-Claude Arnault mwenye umri wa miaka 72, ni mume wa mwanachama wa bodi ya academy ya Sweden, alipatwa na hatia mapema mwezi huu (3 disemba 2018) wa mashtaka mawili ya ubakaji.

Alipewa hukumu ya miaka mbili na nusu gerezani kwa uhalifu huo na, wanachama wanane wa bodi hiyo wame jiuzulu au kujitenga na bodi hiyo kwa sababu ya kashfa hiyo.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service