Shambulio kwa uwanja wa mafuta, lasababisha ongezo ya bei ya mafuta

Viwanja vya mafuta vya Saudi Arabia vya shambuliwa kwa moto

Viwanja vya mafuta vya Saudi Arabia vya shambuliwa kwa moto Source: Reuters

Soko za dunia zina endelea kushuhudia ongezeko la bei ya mafuta, kufuatia shambulizi la viwanda vya mafut nchini Saudi Arabia wekendi iliyopita.


Wachambuzi wamesema waendesha magari wa Australia watalipa zaidi katika vituo vya mafuta, katika siku zijazo na wameonya kuwa, hiyo ni ongezeko ya bei ambayo itaendelea kuongezeka kwa muda mrefu.

Australia ina petroli na mafuta ambayo hayaja safishwa kutumiwa nchini kwa muda wa siku 28, ambayo ni kidogo kama inavyo takiwa katika makubaliano yakimataifa, ambayo yanahitaji nchi kuwa na mafuta yakutosha kutumiwa kwa muda wa siku 90.

Mwezi jana Angus Taylor ali thibitisha kuwa Australia inafanya mazungumzo na marekani, kutumia petroli yake iliyo hifadhiwa.

Wakati huo huo chama cha Labor kimesema kuwa hiyo sio suluhu fanisi kwa usalama wa mafuta, kwa sababu haitapiga jeki usambazaji wa mafuta nchini.

Mbunge huru Andrew Wilkie amesema ni udanganyifu kuwasilisha mpango kama suluhu, wakati unategemea sana wema na hautoi maelezo kuhusu uhaba kimataifa.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service