Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

'Moja ya siku mbaya ya New Zealand' baada ya misikiti kushambuliwa mjini Christchurch

Shambulizi katika misikiti mjini Christchurch

Shambulizi katika misikiti mjini Christchurch Source: AAP

Waziri Mkuu wa New Zealand amesema mashambulizi kwa bunduki mjini Christchurch, kuwa yame sababisha moja ya siku mbaya zaidi nchini New Zealand.


Published

Updated

By Sunil Awasthi

Presented by Gode Migerano

Source: SBS




Share this with family and friends


Waziri Mkuu wa New Zealand amesema mashambulizi kwa bunduki mjini Christchurch, kuwa yame sababisha moja ya siku mbaya zaidi nchini New Zealand.


Taifa hilo liko katika hali ya mshtuko baada ya watu kadhaa kuuawa na wengine kujeruhiwa, baada ya mshambuliaji kumimina risasi kadhaa ndani ya misikiti miwili katika eneo la kusini la mji huo.

Polisi wame sema wame wakamata watu wanne tayari, watatu ni wanaume na mwanamke mmoja ambao wako mbaroni sasa, pamoja naku weka magari kadhaa yaliyo kuwa na vilipuzi chini ya udhibiti wao.

Waziri Mkuu wa Australia Scott Morrison, amethibitisha kuwa mmoja wa wanaume ambao wame wekwa kizuizini ni raia wa Australia, pamoja nakusema kuwa mwanaume huyo ni "gaidi wa mrengo wakulia".

Shirikisho la halmashauri zaki Islamu za Australia, lime toa mawazo na maombi kwa waathiriwa, wahanga, familia zao pamoja na watu wa New Zealand.

Dr Rateb Jneid ndiye rais wa shirika la Muslims Australia, amehamasisha misikiti yote pamoja na sehemu zote za ibada nchini Australia kuwa angalifu zaidi, nakwa wanachama wa jamii yawaislamu kuwa makini zaidi kuhusu usalama wao katika siku zijazo.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now