'Moja ya siku mbaya ya New Zealand' baada ya misikiti kushambuliwa mjini Christchurch

Shambulizi katika misikiti mjini Christchurch

Shambulizi katika misikiti mjini Christchurch Source: AAP

Waziri Mkuu wa New Zealand amesema mashambulizi kwa bunduki mjini Christchurch, kuwa yame sababisha moja ya siku mbaya zaidi nchini New Zealand.


Taifa hilo liko katika hali ya mshtuko baada ya watu kadhaa kuuawa na wengine kujeruhiwa, baada ya mshambuliaji kumimina risasi kadhaa ndani ya misikiti miwili katika eneo la kusini la mji huo.

Polisi wame sema wame wakamata watu wanne tayari, watatu ni wanaume na mwanamke mmoja ambao wako mbaroni sasa, pamoja naku weka magari kadhaa yaliyo kuwa na vilipuzi chini ya udhibiti wao.

Waziri Mkuu wa Australia Scott Morrison, amethibitisha kuwa mmoja wa wanaume ambao wame wekwa kizuizini ni raia wa Australia, pamoja nakusema kuwa mwanaume huyo ni "gaidi wa mrengo wakulia".

Shirikisho la halmashauri zaki Islamu za Australia, lime toa mawazo na maombi kwa waathiriwa, wahanga, familia zao pamoja na watu wa New Zealand.

Dr Rateb Jneid ndiye rais wa shirika la Muslims Australia, amehamasisha misikiti yote pamoja na sehemu zote za ibada nchini Australia kuwa angalifu zaidi, nakwa wanachama wa jamii yawaislamu kuwa makini zaidi kuhusu usalama wao katika siku zijazo.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service