Ongezeko la ugonjwa wa kisukari: Uchunguzi waangazia mwenendo wakutisha wa afya

Blood glucose measurement

A blood glucose measurement is being performed on July 28, 2020 in Pfullendorf, Germany. (Photo by Harry Langer/DeFodi Images via Getty Images) Source: Getty / Getty Images Europe

Serikali kwa sasa inazingatia mawasilisho kwa uchunguzi wa shirikisho, kuhusu ugonjwa wa kisukari, hali ambayo inazidi kuongezeka kote nchini Australia.


Baadhi ya vikundi kama wanawake wajawazito, wa Australia wa kwanza na watu wanao ishi katika vijiji nchini Australia hubeba mzigo mzito zaidi.

Zaidi ya idadi yawa Australia milioni 1.3, kwa sasa wanaishi na ugonjwa wa kisukari kwa maana ya mtu 1 katika watu 20 miongoni mwetu. Na takwimu hiyo inaendelea kuongezeka.

Kati ya mwaka wa 2000 na 2021, idadi ya watu walio kuwa waki ishi na ugonjwa wa kisukari ulikaribia kuongezeka mara tatu kutoka idadi ya watu 460,000 hadi watu milioni 1.3.

Katika mwezi wa Mei, serikali ilizindua uchunguzi bungeni kwa ugonjwa wakisukari, kwa ajili yaku elewa vizuri zaidi tatizo hili linalo ongezeka.

Shirika la National Rural Health Alliance linataka uwekezaji mwingi zaidi utolewe kwa uelewa, kutambua pamoja na miradi yakuzuia.

Mawasilisho kwa kamati hiyo ya uchunguzi kwa ugonjwa wakisukari kwa sasa yamefungwa, tarehe ya lini ripoti ya mwisho kwa uchunguzi hiyo ita tolewa, bado haija tangazwa.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service