Waziri Mkuu Malcolm Turnbull amekuwa akiuza mpangilio mpya wakuhamisha wakimbizi Marekani, ila hajataja idadi ya wakimbizi hao watatumwa, au hata kama mpangilio huo utapona utawala wa Donald Trump utakao anza rasmi mwezi Januari mwaka kesho.
Waziri Mkuu amesema mkataba huo uliafikiwa na utawala wa Obama miezi kadhaa iliyo pita na swala hilo, halija jadiliwa na Bw Trump.
Bw Turnbull ameongezea kuwa serikali ina jadiliana na utawala mmoja kuhusu mpango huo.
Share
