Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Vyama vidogo kuwa mwiba kwa Waziri Mkuu tena

Bango la kampeni la Bi Lucy Gichuhi
Bango la kampeni la Bi Lucy Gichuhi Source: Family First Australia

Matokeo ya uchaguzi mkuu nchini Australia yanapo endelea kutangazwa, SBS Swahili ilizungumza na Bi Lucy Gichuhi, mgombea wa chama cha Family First ndani ya Seneti katika mkoa wa Kusini Australia. Bi Lucy alizungumzia mchakato wa kampeni pamoja na hatua yake yaku gombea kiti katika seneti.


Published

Updated

By SBS Swahili

Source: SBS



Share this with family and friends


Matokeo ya uchaguzi mkuu nchini Australia yanapo endelea kutangazwa, SBS Swahili ilizungumza na Bi Lucy Gichuhi, mgombea wa chama cha Family First ndani ya Seneti katika mkoa wa Kusini Australia. Bi Lucy alizungumzia mchakato wa kampeni pamoja na hatua yake yaku gombea kiti katika seneti.


Wiki chache kabla ya uchaguzi mkuu, Waziri Mkuu wa Australia kwa ushirikiano na chama cha Australian Greens ali pitisha mswada bungeni ambao lengo lake lilikuwa kupunguza uwezekano wa wagombea huru na vyama vidogo kupata kura zakutosha kuingia bungeni.

Hatua hiyo ilichukuliwa kwa sababu ya matatizo ambayo serikali ilikuwa ikikabiliana nayo kutoka kwa baadhi ya wabunge huru na vyama vidogo ambavyo mara nyingi huwa havi pitishi miswada ya serikali.

Hata hivyo wapiga kura wame toa kura zao kwa wagombea huru na vyama vidogo, hatua ambayo itaendelea kuwa mwiba kwa Waziri Mkuu.

 


Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now