Polisi wa Victoria wamehaidi kuchukua hatua dhidi ya matendo yoyote ya unyanyasaji dhidi ya jamii za Waislamu, baada ya shambulizi la tarehe 9 Novemba 2018 katika mtaa wa Bourke, ambako kisu kilitumiwa katika shambulizi hilo katikati ya mji wa Melbourne.
Maafisa wa ngazi za juu wamesema kuwa, wanawake wanaovaa hijabu wamekuwa wakitukanwa katika umma, baada ya shambulizi hilo lililofanywa na mwanaume aliyezaliwa Somalia. Idara hiyo ya Polisi imetupilia mbali pia, mapendekezo kuwa motisha ya mshambuliaji huyo, ilikuwa kile ambacho kimeripotiwa kuwa ni itikadi kali za kiislamu.
Watu wa Melbourne wametoa heshima zao za mwisho leo jumanne tarehe 20 Novemba 2018, kwa marehemu Sisto Malaspina ambaye alikuwa mmiliki wa mgahawa maarufu kwa jina la Pelligrini's.
Umma ulijumuika ndani ya kanisa la Saint Patricks, kumuaga marehemu Sisto, katika ibada iliyosimamiwa na serikali ya Victoria.
Share






