Polisi wajumuika na jamii ya Wasomali baada ya shambulizi la mtaa wa Bourke

Mhanga wa shambulizi la kisu katika mtaa wa Bourke, mjini Melbourne, Victoria

Mhanga wa shambulizi la kisu katika mtaa wa Bourke, mjini Melbourne, Victoria Source: AAP

Polisi wa Victoria wamehaidi kuchukua hatua dhidi ya matendo yoyote ya unyanyasaji dhidi ya jamii za Waislamu, baada ya shambulizi la tarehe 9 Novemba 2018 katika mtaa wa Bourke, ambako kisu kilitumiwa katika shambulizi hilo katikati ya mji wa Melbourne.


Maafisa wa ngazi za juu wamesema kuwa, wanawake wanaovaa hijabu wamekuwa wakitukanwa katika umma, baada ya shambulizi hilo lililofanywa na mwanaume aliyezaliwa Somalia. Idara hiyo ya Polisi imetupilia mbali pia, mapendekezo kuwa motisha ya mshambuliaji huyo, ilikuwa kile ambacho kimeripotiwa kuwa ni itikadi kali za kiislamu.

Watu wa Melbourne wametoa heshima zao za mwisho leo jumanne tarehe 20 Novemba 2018, kwa marehemu Sisto Malaspina ambaye alikuwa mmiliki wa mgahawa maarufu kwa jina la Pelligrini's.

Umma ulijumuika ndani ya kanisa la Saint Patricks, kumuaga marehemu Sisto, katika ibada iliyosimamiwa na serikali ya Victoria.

 


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service