Polisi Tanzania imesema Ijumaa walikuwa wanachunguza madai dhidi ya baadhi ya maafisa wa polisi, kuhusika na ubakaji na udhalilishaji wa kingono wa wanawake kadhaa katika vilabu vya usiku.
Madai hayo yamelitikisa jeshi la polisi la Tanzania, hatua ambayo imepelekea mashirika kadhaa ya utetezi wa haki za binadam kutaka uchunguzi wa haraka kufunywa dhidi ya wahusika.
Shutuma hizo zilitolewa wakati wa mkutano wa hadhara, na kamishna wa polisi wa wilaya ya Handeni, katika mkoa wa Tanga wiki iliyopita.
Mwandishi wetu Jason Nyakundi ame andaa maelezo zaidi.
Share






