Serikali ya Morrison inaendelea kupoteza ushawishi, kwa mpango wake waku lazimisha vipimo vya mihadarati kwa wapokeaji wa malipo ya ustawi, baada ya seneta huru Jacqui Lambie kuzua wasi wasi kuhusu uhaba wa huduma zinazo ungwa kwa mpango huo.
Kwa upande wake, chama cha Labor kilitumia kikao cha kwanza cha bunge, baada ya mapumziko ya wiki tano, kuishinikiza serikali kwa hali ya uchumi wa taifa.
Serikali imeahidi kuunda tume ya uadilifu ila, kwa chama cha Labor na wabunge huru, pendekezo hilo halitoshi.
Share





