Prof Kitwaja: "Afrika lazima ijipange vizuri ili inufaike kupitia uhusiano wake na Marekani"

US Africa .jpg

WASHINGTON, DC - DECEMBER 14: U.S. President Joe Biden delivers remarks at the U.S. - Africa Leaders Summit on December 14, 2022 in Washington, DC. The Summit brings together heads of state, government officials, business leaders, and civil society to strengthen ties between the U.S. and Africa. Credit: Kevin Dietsch/Getty Images

Mkutano wa Viongozi wa Marekani na Afrika, ulikuwa na mambo mengi ya kuridhisha na makubwa, malengo ya bilioni ya dola, pamoja na taarifa kwamba rais wa Marekani atalitembela bara hilo.


Alipo hojiwa kuhusu mkutano huo, Prof Kitwaja kutoka chuo cha Arusha alionya kwamba "Afrika lazima ijipange vizuri ili inufaike kupitia uhusiano wake na Marekani".

Katika taarifa zingine kutoka bara la Afrika, bunge la Msumbiji limeidhinisha mswaada wa sheria inayohalalisha kujihusisha kwa wanamgambo katika vita dhidi ya wapiganaji wa Kiislamu katika jimbo la kaskazini la Cabo Delgado. Wanamgambo wa jimbo hilo wamekuwa wakisaidia jeshi na washirika wao kutoka Rwanda na Jumuia ya maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika katika vita dhidi ya wapiganaji wa kislamu katika jimbo hilo.

Na nchini Uganda, Rais Museveni, ameondoa vizuizi vyote vinavyohusiana na Ebola, akisema kuwa nchi hiyo ya Afrika Mashariki imepiga hatua katika kukabiliana na ugonjwa huo hatari. Museveni amefuta vizuizi vyote vilivyowekwa katika wilaya ya Mubende, ambayo ndio ilikuwa kitovu cha ugonjwa huo, kulikoshuhudiwa visa 66 vya maambukizi na vifo 29, na katika eneo la Kassanda lililokuwa na visa 49 na vifo 21.

Bonyeza hapo juu kwa taarifa zaidi kwa mwandishi wetu Jason Nyakundi.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service