Ramadan yaanza- na ulinzi waimarishwa

Waumini washiriki katika sala ya Ramadan

Waislam nchini Indonesia washiriki katika sala ya jioni la 'tarawih', jioni ya kwanza ya mwezi wa Ramadan, ndani ya msikiti wa Istiqlal mjini Jakarta,Indonesia Source: AAP

Waislamu duniani kote wame anza mafungo, katika mwezi mtukufu wa Ramadan ambao ni mwezi muhimu katika kalenda ya waislamu.


Hatakama taratibu nyingi za mafungo zina ambatana na mazoea ya msingi, baadhi ya taratibu hizo zina tofautiana kulingana na sehemu ambako mtu yuko.

Mafungo ya Ramadan ya mwaka huu, yamejiri miezi michache tu baada ya mashambulizi katika misikiti ya mji wa Christchurch, ambayo yamesababisha misikiti mingi nchini Australia kuongeza ulinzi wao.

Masaa ya Australia hufanya mafungo ya Ramadan kuwa rahisi, wengi wao mwaka huu watafanya mafungo, kwa muda wa masaa 12 kwa siku pekee.

Baadhi yawatu barani Ulaya watakuwa na jua kwa muda mrefu kidogo kila siku, kumaanisha itawabidi wafanye mafungo kwa muda wa masaa 19. Kuna wakati katika mwaka ambapo, katika sehemu chache ambazo ziko juu ya eneo la duru la arctic, ambako jua huwa halitui.

Katika visa kama hivyo, mamlaka wame toa mwongozo kuwa, waislamu wanaweza funga sawa na nchi ya kiislamu ambayo iko karibu yao, au sambamba na Mecca, Saudi Arabia ambako Uislamu ulizaliwa.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service