Uongozi wa Rais Evariste Ndayishimiye wa Burundi, umeanza chini ya wingu la kifo cha ghafla cha rais Peter Nkurunziza, pamoja na wimbi la matarajio mengi kutoka kwa raia wa taifa hilo.
Katika mazungumzo maalum wakati wa kongamano lakutoa heshima za mwisho kwa marehemu Rais Peter Nkurunziza, mwanachama wa jamii yawarundi Rosalia, ameihamasisha serikali mpya ya Jenerali mstaafu Evariste Ndayishimiye, ichukulie hatua kali unyanyasaji wakijinsia wa wanawake nchini Burundi.
Mwanachama huyo aliomba pia wanawake pamoja na wanaume nchini Burundi, wasaidiwe kupata mitaji ambayo itawawezesha kufanya biashara ndogo ndogo, ili nao wachangie katika uchumi taifa pamoja nakuendeleza familia zao.
Share





