Unaweza sikiza makala ya Idhaa ya Kiswahili ya SBS, yanayo peperushwa kati ya saa nne na saa tano kila usiku wa Jumapili bila matangazo au miziki.
Katika makala ya leo kuna:
Taarifa mpya za habari za Australia, na kutoka Afrika Mashariki na Kati.
Makala kuhusu jinsi yakutumia namba ya huduma ya dharura ya 000 nchini Australia.
Mahojiano na Bw Alfred Koech, mwanariadha mstaafu mwenye asili ya Kenya. Bw Koech alizungumzia sakata lakucheleweshwa kwa vibali vya usafiri vya mwanariadha mashuhuri wa mbio za mita 100 Ferdinand Omanyala kabla ya kuanza kwa mashindano ya riadha Oregon, Marekani. Bw Koecha alizungumzia jinsi tukio kama hilo linavyo weza mdhuru mwanariadha kimwili, kisaikolojia pamoja na madhara hayo kuwa athiri wandani wa mhusika.
Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.
Share






