Umiliki wa nyumba ni moja ya ndoto zawa Australia wote, ila kwa wengi wao hali hiyo itasalia kuwa ndoto tu.
Serikali ya shirikisho imekiri kuwa wa Australia wengi wanalemewa na swala laku nunua nyumba yao ya kwanza.
Alipozungumzia swala hili, mweka hazina wa taifa Scott Morrison amesema kwamba bei ya nyumba inaweza pungua iwapo nyumba zitapatikana kwa urahisi.
Bw Morrison amelaumu kanuni tata za mipango, kwaku ongeza bei ya nyumba. Amezihamasisha pia serikali za majimbo, kuachia ardhiya ziada kwa ajili yaku rahisisha tatizo hilo.
Share
