Serikali ya shirikisho imetoa jibu kwa ripoti ya tume ya kamishna wa ubaguzi wa jinsia, kuhusu heshima kazini baada ya zaidi ya miaka mbili. Jibu hilo limepokewa kwa hisia mseto.
Jibu la serikali limejiri inapo kabiliwa kwa shinikizo ishughulikie usalama wa wanawake, baada ya madai kadhaa ya ubakaji na unyanyasaji wakijinsia.
Waziri wa usalama wa wanawake Anne Ruston anawahamasisha watu wajisajili kwa kongamano la usalama wa wanawake la Julai, na wawasilishe mawazo yao.
Kongamano lakitaifa la usalama wa wanawake, limeratibiwa kufanyika tarehe 29 na 30 Julai 2021.
Share






