Socceroos waingia katika mechi ya mwisho ya kombe la dunia kwa matumaini mengi, ila wata hitaji msaada

Mashabiki wa Socceroos wakitazama mechi ya timu ya taifa ya Australia

Mashabiki wa Socceroos wakitazama mechi ya timu ya taifa ya Australia. Source: AAP

Kampeni ya kombe la dunia ya Australia ime ingia katika dakika za lala salama, Socceroos wana hitaji zaidi matokeo ambayo ni zaidi ya ushindi leo, iwapo wata baki katika michuano hiyo.


Australia iki pata ushindi dhidi ya Peru, Denmark lazima ishindwe dhidi ya Ufaransa, kuwapa Socceroos fursa yaku endelea katika hatua ya mchujo.

Hata hivyo, kila kitu hakijawa sambamba kwa upande wa mechi hizo.

Hatma ya safari ya Australia na Denmark katika kombe la dunia, huenda ika amuliwa kupitia magoli.

Iwapo Australia itashinda mechi yake, na Denmark ishindwe dhidi ya Ufaransa, magoli kati ya timu hizo mbili yata tumiwa kuamua timu itakayo endelea katika hatu ya mchujo.

Australia ina ingia katika mechi hiyo, ikiwa imefunga magoli mawili, nakufungwa magoli matatu. Ilhali Denmark, imefunga magoli mawili nakufungwa moja.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service